Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 20 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 179 2022-05-11

Name

Bahati Khamis Kombo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani na eneo lililoachwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania katika Shehia ya Kengeje – Pemba?

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI (K.n.y. NAIBU WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bahati Khamis Kombo, Mbunge kutoka Baraza la Wawakilishi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ilivyo katika maeneo mengine, Serikali imeendelea kulitumia eneo lililotajwa la Shehia ya Kengeje, Kusini Pemba kwa ajili ya kuimarisha ulinzi wa Kisiwa cha Pemba upande wa Magharibi. Vilevile eneo hilo linatumika kufanyia mafunzo, ambayo ni muhimu katika kuliimarisha Jeshi.

Hadi sasa eneo hilo linakaliwa na kiteule cha Jeshi 14KJ. Nitoe rai kwa wananchi kuendelea kushirikiana na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, kwa kutambua kuwa ulinzi wa nchi yetu pamoja na maeneo ya Jeshi ni jukumu la kila mwananchi. Ahsante.