Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 20 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 176 2022-05-11

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itafikisha umeme katika Kata mbili ambazo hazijawahi kupata umeme kabisa katika Jimbo la Ndanda?

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Cecil David Mwambe, Mbunge wa Ndanda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika Jimbo la Ndanda kuna Kata 16 ambapo Kata mbili (2) kati ya Kata hizo hazina umeme. Kata hizo ni Msikisi na Mpanyani. Aidha, Kata ya Msikisi inaundwa na vijiji vya Miwale, Namalembo na Msikisi yenyewe, wakati Kata ya Mpanyani inaundwa na vijiji vya Nambawala A, Nambawala B, Mhima, Muungano na Mpanyani yenyewe.

Mheshimiwa Naibu Spika, Vijiji hivyo vyote vya Kata hizo vinapatiwa umeme kupitia mradi wa REA Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili ulioanza kutekelezwa na Mkandarasi M/s Namis Corporate Engineers and Contractors mwezi Aprili, 2021 na unatarajia kukamilika Desemba, 2022.