Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 20 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 175 2022-05-11

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE ASIA A. HALAMGA K.n.y. MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: -

Je, ni nini kauli ya Serikali juu ya kusajili na kuboresha miundombinu ya Shule Shikizi zilizojengwa kwa nguvu za Wananchi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Edward Kisau Olelekaita, Mbunge wa Jimbo la Kiteto kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, vituo shikizi ni vituo vilivyojengwa kwenye maeneo ambayo hayana shule au shule ziko umbali mrefu kutoka kwenye maeneo wanayoishi wananchi. Vituo hivi kabla ya kusajiliwa kuwa shule kamili hufanyiwa ukaguzi na ufuatiliaji na Wathibiti Ubora wa Shule kwa kushirikiana na Maafisa kutoka ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri. Kama hakuna mapungufu taarifa ya ukaguzi pamoja na barua ya kuomba usajili hutumwa kwa Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ili Shule husika ipate usajili.

Mheshimiwa Spika, ili vituo shikizi viweze kusajiliwa na kuwa shule halmashauri pamoja na wananchi wa vijiji husika wayafanyie kazi maelekezo ya wathibiti ubora wa shule ili shule hizo ziweze kupata usajili.