Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 19 Water and Irrigation Wizara ya Maji 168 2022-05-10

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Mradi wa Maji wa Kintinku- Lusilile katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Manyoni Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Maji Kintinku-Lusilile ni mradi uliopangwa kuhudumia Vijiji 11 vya Chikuyu, Mwiboo, Mbwasa, Makutupora, Mtiwe, Chilejeho, Maweni, Mvumi, Ngaiti, Kintinku na Lusilile. Mradi huo unatekelezwa kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza ilikamilika mwezi Oktoba, 2021 na Vijiji vitatu vya Chikuyu, Mwiboo na Mbwasa vinapata huduma ya maji. Katika mwaka wa fedha 2022/ 2023, utekelezaji wa awamu ya pili ya mradi unaendelea na unatarajiwa kukamilika mwezi Oktoba, 2022 na kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji katika vijiji vyote 11.