Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 18 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 159 2022-05-09

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA aliuliza: -

Je, Serikali kupitia Tume ya Ushindani (FCC) ina mkakati gani wa kumlinda mlaji katika biashara za mtandaoni?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Judith Salvio Kapinga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha biashara ya mtandaoni inalindwa, Tume ya Ushindani (FCC) ina Mpango mkakati wa kutekeleza jukumu la kumlinda mlaji wa biashara mtandaoni 2021/2022 - 2025/2026. Mkakati huo ni kupitia njia ya elimu kwa walaji kuhusu haki na wajibu wao na mambo ya msingi ya kuzingatia wakati wakifanya biashara za mtandaoni ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa taarifa zilizotolewa kwenye mtandao kuwa ni sahihi. Nakushukuru.