Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 18 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 158 2022-05-09

Name

Ali Hassan Omar King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Jang'ombe

Primary Question

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN K.n.y. MHE. ALI HASSAN OMAR KING aliuliza: -

Je, TRA itasitisha lini kukusanya na kuzirudisha fedha za VAT ilizokusanya kutoka kwenye miamala ya mtandaoni iliyofanywa Zanzibar?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ali Hassan Omar King, Mbunge wa Jimbo la Jang’ombe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria za Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwa pande zote mbili za Muungano zimeweka msingi wa kutoza na kukusanya VAT pale ambapo huduma inapotolewa. Kwa muktadha huo, huduma ikitolewa Tanzania Bara, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inatoza VAT ya asilimia 18 kwa mujibu wa Sheria ya VAT inayotumika Tanzania Bara na huduma ikitolewa Zanzibar, Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) inatoza VAT ya asilimia 15 kwa mujibu wa Sheria ya VAT inayotumika Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kutambua sehemu ambapo huduma imetumika, Serikali za pande zote mbili za Muungano ziliunda mfumo wa kielektroniki ujulikanao kama Electronic Revenue Collection System (e-RCS) wenye uwezo wa kutambua miamala yote inavyofanyika na hivyo kusaidia kutunza takwimu sahihi za mauzo yanayotokana na miamala ya mitandao inayofanywa na watumiaji wa kila upande. Mfumo huu unasimamiwa na kamati ya wataalam wa kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB).

Mheshimiwa Mwenyekiti, mifumo ya kampuni zote za simu hapa nchini imeunganishwa na mfumo wa Serikali wa e-RCS na taarifa za miamala ya mitandao hutolewa kila mwezi ikiainisha bayana huduma zilizotumika Tanzania Bara na zile zilizotumika Zanzibar. Ahsante.