Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 17 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 149 2022-05-06

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SYLVIA F. SIGULA aliuliza:-
Je, ni lini ujenzi wa madarasa katika Kampasi ya Chuo cha Uvuvi Kibirizi utaanza?

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sylvia Francis Sigula, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wakala wa Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kupitia kampasi ya Kibirizi ulianza kutoa mafunzo ya muda mrefu ya tasnia ya uvuvi mwaka 2013/2014 kwa kutumia majengo ya kilichokuwa Kiwanda cha Mashua Kigoma ambacho kilikuwa katika eneo la Kibirizi. Hivyo, kwa sasa kampasi ya Kibirizi inatoa mafunzo ya teknolojia ya ukuzaji viumbe maji (aquaculture technology) katika ngazi za Astashahada na Stashahada kwa kutumia madarasa yaliyopo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuimarisha Kampasi ya Kibirizi kwa kujenga madarasa mapya na kuipatia vitendea kazi ili iweze kutoa mafunzo zaidi ikiwemo masomo ya sayansi na teknolojia ya uvuvi (fisheries science and technology) na usimamizi wa uvuvi (fisheries management) ngazi za Astashahada na Stashahada, ahsante.