Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 17 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 147 2022-05-06

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha Mkoa wa Rukwa unalima zao la maharage ya soya lenye uhitaji mkubwa zaidi duniani?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege, Mbunge wa Kalambo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Rukwa ni moja ya mikoa inayozalisha maharage ya soya kwa wingi nchini kwa ajili ya chakula na biashara. Katika mwaka 2020/2021 mkoa ulizalisha jumla ya tani 121,356 katika eneo la hekta 120,432. Mwaka 2021/2022 mkoa umelenga kuzalisha jumla ya tani 128,672 za maharage katika eneo la hekta 121,961.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuendeleza kilimo cha maharage ya soya Mkoani Rukwa, Serikali kwa kushirikiana na wadau imechukua hatua mbalimbali ikiwemo kuimarisha upatikanaji wa mbegu bora za maharage ya soya nchini kupitia sekta binafsi, Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI-Uyole) na Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) na kupitia vikundi vya wakulima wazalishaji wa mbegu za daraja la kuazimiwa ubora (QDS) na kutoa mafunzo ya uzalishaji wa maharage ya soya kwa Maafisa Ugani 64 katika ngazi ya Halmashauri, kata na vijiji ili kuwezesha wakulima kuzalisha kwa tija.

Mheshimiwa Naibu Spika, Maafisa Ugani hao wanatumika katika kutoa ushauri na kuandaa mashamba ya mfano ya kilimo cha maharage ya soya katika maeneo yao, kupima afya ya udongo ili kuwezesha matumizi sahihi ya pembejeo za kilimo, kuhamasisha kilimo cha mkataba kati ya wakulima na wanunuzi ili kuwa na uhakika wa soko la mazao ya wakulima wanaolima maharage ya soya nchini.