Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 17 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 140 2022-05-06

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:-
Je, kwa nini Serikali isipitishe mkakati maalum kwenye bajeti ya mwaka 2022/2023 wa kujenga shule za msingi kwenye vitongoji vyote vyenye watoto zaidi ya 200?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph George Kakunda, Mbunge wa Jimbo la Sikonge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, maelekezo ya Serikali ni kuwa na Shule ya Msingi kila Kijiji ikiwemo na vitongoji katika jimbo la Sikonge.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na ukweli kuwa Jimbo la Sikonge kwa sasa halina shule za msingi za kutosha, Halmashauri ya Sikonge kupitia fedha toka Serikalini na kwa kutumia vyanzo mbalimbali vya mapato vya Halmashauri inaendelea kuhimiza wananchi, jamii na wadau wa maendeleo kujenga miundombinu ya shule za msingi ili kukidhi mahitaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kutenga fedha kwa ajili ya kujenga shule za msingi kila kitongoji kutategemeana na hali ya uchumi wa nchi na upatikanaji wa fedha. Hata hivyo, kwa jinsi sera ilivyo hatujafikia hatua ya kujenga shule kwa kila kitongoji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa shughuli ya ujenzi wa shule inawahusisha wananchi na jamii kwa ujumla, napenda kumshauri Mheshimiwa Mbunge kuendelea kushirikiana na wananchi na Halmashauri kujenga shule katika kila kijiji ili kuwezesha wanafunzi wote wenye umri wa kwenda shule kuweza kupata nafasi.