Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 15 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 128 2022-04-29

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: -

Je, Serikali haioni ni kuwakandamiza Wananchi wa Itigi kwa kuondoa Miji kwenye bei ya kuweka umeme kutoka shilingi 27,000 hadi shilingi 320,000?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI aljibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali haikandamizi mwananchi yoyote, bali inawajali na kuwaunganishia huduma ya umeme kwa gharama zenye ruzuku ndani yake. Kati ya mwaka 2008 na 2013, gharama za kuunganisha umeme zilikuwa shilingi 455,104.76 ndani ya mita 30; shilingi 1,351,883.52 ndani ya mita 70; na shilingi 2,001,421.60 ndani ya mita 120 kwa maeneo ya Mijini na Vijijini. Gharama hizi ndizo zilizokuwa zinaakisi gharama halisi za kuunganisha umeme wa njia moja.

Mheshimiwa Spika, Mwaka 2013, Serikali ilipunguza kwa kuweka ruzuku gharama za kuunganisha umeme kuwa shilingi 320,960.00 ndani ya mita 30, shilingi 515,617.52 ndani ya mita 70 na shilingi 696,669.64 ndani ya mita 120 kwa maeneo ya mijini. shilingi 177,000.00 ndani ya mita 30, shilingi 337,739.60 ndani ya mita 70 na shilingi 454,654.00 ndani ya mita 120 kwa maeneo ya vijijini.

Mheshimiwa Spika, kuanzia mwezi Januari, 2022 bei imerejea kwenye gharama za mwaka 2013 kwa maeneo ya mijini na shilingi 27,000 kwa maeneo ya vijijini. Gharama hizi zina ruzuku ya Serikali ndani yake. TANESCO inabaini eneo la miji na vijiji kwa kutumia Sheria ya Mipango Miji Namba 8 ya mwaka 2007.