Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 15 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 122 2022-04-29

Name

Agnesta Lambert Kaiza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNESTA L. KAIZA aliuliza: -

Je, Serikali imefikia hatua gani katika utekelezaji wa mradi wa kuzuia mafuriko katika Mto Msimbazi?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu Muungano na Mazingira, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Agnes Lambert Kaizer, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mradi huu kwa sasa uko katika hatua za kufanya uhakiki wa taarifa na mali za wananchi wanaopaswa kupokea fidia na kusainiwa kwa mkataba baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Benki ya Dunia. Mradi huo unategemewa kuanza rasmi mwezi Julai, 2022.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira inaamini kuwa utekelezaji wa mradi huu utawezesha kuondoa kabisa tatizo la mafuriko katika Bonde la Mto Msimbazi.