Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 13 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 99 2022-04-27

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMANI A. MAIGE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itabadilisha mtambo wa kutengeneza hewa ya Naitrojeni Kituo cha Afya Upuge na kuleta mtambo wa hewa ya Oksijeni?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Athumani Almas Maige, Mbunge wa Jimbo la Tabora Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya Upuge kilifungiwa mtambo wa kutengeneza vacuum mwaka 2012 kwa ajili ya huduma za dharura na upasuaji. Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022 imefanya tathmini ya mitambo hiyo na matengenezo madogo ya kuzibua njia ya hewa yatafanyika ili iweze kutumika.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO-19 katika mwaka wa fedha 2021/2022 imepanga kununua mitambo 10 ya kuzalisha hewa ya Oksijeni . Mitambo hiyo itazalisha hewa na kusambaza kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ikiwemo Kituo cha Afya cha Upuge ambacho kimefungiwa mfumo wa kupokea na kutawanya hewa ya Oksijeni. Ahsante.