Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 11 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 95 2022-04-22

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza vyanzo vya mitaji kwa akina Mama wajasiriamali mbali ya fedha zinazotolewa na Halmashauri?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu Swali la Mheshimiwa Esther Lukago Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikiwawezesha kimtaji akina mama kupitia Mifuko ya Uwezeshaji inayoratibiwa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Serikali ilianzisha Mifuko hii ili kuwasaidia wananchi wake hasa makundi maalum kwa lengo la kupunguza changamoto ya upatikanaji wa mitaji yenye masharti nafuu.

Mheshimiwa Spika, vilevile, Serikali ilianzisha Benki ya Wanawake Tanzania na ili kuboresha huduma shughuli za Benki hiyo zilihamishiwa katika Benki ya Tanzania Postal Bank sasa hivi inaitwa Tanzania Commercial Bank. Aidha, katika mwaka wa fedha wa 2020/2021 Benki hiyo kupitia dirisha la wanawake imeendelea kutoa mikopo kwa wanawake, ambapo kiasi cha Shilingi Bilioni 22.3 kimetolewa kwa wanawake 6,327. Nakushukuru.