Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 9 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 76 2022-04-20

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatoa vibali vya kuajiri Walimu wa kutosha kukabiliana na ongezeko la Wanafunzi na Wahitimu wangapi wapo kwenye soko la ajira?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. David Mathayo David Mbunge wa Same Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2021/2022 Serikali imetoa kibali cha nafasi 10,003 za ajira kwa Walimu. Aidha, katika Mwaka wa Fedha 2022/2023 Serikali imepanga kutoa kibali cha ajira kwa nafasi 30,000 zikiwemo nafasi za Walimu.

Mheshimiwa Spika, kuhusu wahitimu waliopo kwenye soko la ajira, ninapenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa, kuanzia mwaka 2016 hadi Desemba, 2020 jumla ya wahitimu ni 248,379. Idadi hii inajumuisha Walimu wa Astashahada, Stashahada na Shahada na kati ya wahitimu hawa wameajiriwa na Serikali na wengine Sekta Binafsi.