Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 9 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 148 2023-02-10

Name

Toufiq Salim Turky

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpendae

Primary Question

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI K.n.y. MHE. TOUFIQ SALIM TURKY aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kusaidia makampuni ya wazawa yenye mikopo katika taasisi za fedha kutokana na athari za UVIKO-19?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Taofiq Salim Turky, Mbunge wa Mpendae kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutekeleza hatua za kiutawala na kibajeti kwa kuwa athari zilizojitokeza za UVIKO-19 zilitokana na kuvurugika kwa mnyororo wa uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa bidhaa na huduma katika nchi washirika wa kibiashara ikilinganishwa na soko la ndani. Aidha, uamuzi huo ulichukuliwa kwa kuwa shughuli zote za kibiashara hapa nchini ziliendelea kama kawaida.

Mheshimiwa Spika, hatua za kiutawala na kibajeti zilizochukuliwa na Serikali ni pamoja na: -

i. Kuiagiza benki na taasisi za fedha kutoa unafuu katika urejeshwaji wa mikopo kwa kuongeza muda wa urejeshwaji wa mikopo.

ii. Kushirikisha sekta binafsi kupitia zabuni za watoa huduma na wakandarasi katika utekelezaji wa Mpango wa Kukabiliana na Athari za UVIKO-19 kwa lengo la kuiwezesha kutengeneza faida na kurejesha mikopo katika benki na taasisi za fedha.

iii. Kutoa kipaumbele kwa malipo ya malimbikizo ya madeni, madai na marejesho ya kodi yaliyohakikiwa ili kuongeza mzunguko wa fedha katika uchumi; na

iv. Kutoa unafuu wa kikodi, ikiwemo kodi ya kuendeleza ufundi stadi kutoka asilimia 4.5 hadi asilimia nne na kupandisha kiwango cha chini cha idadi ya waajiriwa wanaostahili kulipiwa kodi kutoka asilimia nne hadi 10 ili kupunguza gharama za uendeshaji kwa waajiri na hivyo kuwezesha marejesho ya mikopo kwenye benki na taasisi za fedha.

Mheshimiwa Spika, ahsante.