Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 9 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 143 2023-02-10

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE aliuliza: -

Je, ni lini barabara ya Mlowo – Utambalila – Chitete na Utambalila – Kamsamba kilometa 145 inayounganisha Mikoa ya Songwe na Katavi itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa George Ranwell Mwenisongole, Mbunge wa Mbozi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa barabara ya Mlowo – Utambalila – Kamsamba yenye urefu wa kilometa 145 umekamilika mwaka 2020. Ujenzi wa Daraja la Momba lenye urefu wa kilometa 80 lililopo kwenye barabara hii eneo la mpakani mwa Songwe na Rukwa na barabara unganishi zenye urefu wa mita 950 kwa kiwango cha lami umekamilika mwezi Julai, 2019. Baada ya ujenzi wa daraja kukamilika, Serikali inaendelea kutafuta fedha za kuendelea na ujenzi wa barabara hiyo, ahsante.