Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 135 2023-02-10

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatambua mipaka ya Halmashauri ya Mkalama na Iramba ili kuondoa migogoro katika Kata za Tumuli, Kinyangiri na Gumanga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Isack Mtinga, Mbunge wa Jimbo la Iramba Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mgogoro kati ya Kijiji cha Mgungia, Kata ya Maluga, Tarafa ya Kinampanda, Wilaya ya Iramba na Kijiji cha Milade, Kata ya Tumuli, Tarafa ya Kinyangiri Wilaya ya Mkalama ulikuwa ukisababishwa na shughuli za kilimo, ufugaji, pamoja na wananchi kutokuwa na ufahamu wa mipaka yao ya vijiji. Wananchi wa pande zote mbili zenye mgogoro walikubaliana na mipaka iliooneshwa na ndiyo iliyotumika katika zoezi la maandalizi ya Mpango wa Matumizi ya Ardhi.

Mheshimiwa Spika, mgogoro kati ya Kijiji cha Maluga, Kata ya Maluga, Tarafa ya Kinampanda na Vijiji vya Tumuli na Kitumbili, Kata ya Tumuli, Tarafa ya Kinyangiri ulikuwa ukisababishwa na uwepo wa makosa katika ramani za upimaji wa vijiji ya mwaka 2010. Wataalam wamekutana uwandani na kufanikiwa kuonesha mpaka wa kila kijiji kwa mujibu wa Tangazo la Serikali Namba 446 la mwaka 2013 la uanzishwaji wa Wilaya.

Mheshimiwa Spika, mgogoro wa mpaka kati ya Wilaya ya Iramba, Kijiji cha Kisana, Kata ya Kisiriri na Wilaya ya Mkalama Vijiji vya Kinamkamba na Mghimba, Kata ya Gumanga unasababishwa na wananchi wa pande zote mbili kutotambua mipaka yao. Wataalamu wa ardhi na viongozi kutoka Wilaya zote mbili walifika uwandani mnamo tarehe 19 Januari, 2018 na kufanya zoezi la kuhakiki mpaka pamoja na kutoa eimu kwa wananchi juu ya haki ya umiliki wa ardhi na kutii sheria na taratibu zilizowekwa ili kuepusha migogoro, ahsante sana.