Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 9 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 132 2023-02-10

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE aliuliza: -

Je, Serikali haioni haja ya kutoa elimu kwa watumishi juu ya ukokotoaji wa mafao?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Alice Karungi Kaijage, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ili kuhakikisha watumishi wanapata elimu juu ya ukokotoaji wa mafao na elimu ya hifadhi ya jamii kwa ujumla, Serikali kupitia Mifuko ya PSSSF na NSSF imekuwa ikitoa elimu kwa watumishi.

Mheshimiwa Spika, kuanzia mwezi Julai hadi Desemba 2022 mifuko imeweza kutoa elimu kwa jumla ya waajiri 318 ambapo wanachama 19,656 walihudhuria mafunzo hayo kutoka katika sekta ya umma na sekta binafsi. Kazi ya kuwafikia waajiri na wanachama wengine ili kuwapa elimu husika inaendelea.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kusimamia, kuratibu na kuhakikisha elimu kwa watumishi wa umma inatolewa kupitia makundi mbalimbali yanapokuwa na vikao kama Mabaraza ya Wafanyakazi, semina, warsha na makongamano. Aidha, mifuko inaendelea kuwatembelea watumishi katika maeneo yao ya kazi, kuandaa na kuwashirikisha katika vipindi kwenye luninga na kurusha vibango katika mitandao ya kijamii, ahsante.