Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 8 Water and Irrigation Wizara ya Maji 126 2023-02-09

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la maji kwenye Mji Mdogo wa Laela na Mpui katika Jimbo la Kwela?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deus Sangu, Mbunge wa Jimbo la Kwela kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Mji Mdogo wa Laela ni 51%. Ili kuboresha huduma ya maji Laela kwa mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imeendelea na upanuzi wa Mradi wa Maji wa Laela na kazi zinazofanyika ni pamoja na ulazaji wa mabomba yenye urefu wa kilometa 2.6 na ukarabati wa tenki lenye ujazo wa lita 225,000.

Aidha, kwa upande wa Kata ya Mpui yenye vijiji vya Mpui A na Mpui B wananchi wanapata maji kupitia chanzo cha mserereko na kisima na hali ya huduma ya maji ni 36%. Ili kupunguza kero ya maji Kata ya Mpui katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali itachimba kisima kirefu kimoja.

Mheshimiwa Spika, mpango wa muda mrefu wa kumaliza tatizo la maji katika Mji Mdogo wa Laela na Kata ya Mpui, kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali itajenga mradi mkumbwa utakaotumia chanzo cha Ziwa Tanganyika au Mto Momba. Kwa sasa usanifu wa mradi huo unaendelea.