Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 8 Foreign Affairs and International Cooperation Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 124 2023-02-09

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuainisha nchi ambazo fursa za biashara na uwekezaji zinaweza kuiletea nchi yetu mapato na kupandisha pato la Taifa zinapatikana?

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana na kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Felista Njau, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutekeleza dhana ya diplomasia ya uchumi ambayo pamoja na mambo mengine ni kukuza biashara na uwekezaji toka nchi mbalimbali. Dhana hii inahusisha Sekta mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Wizara za kisekta na Balozi zetu imeendelea kutangaza fursa za kibiashara na uwekezaji zenye manufaa kwa Taifa letu. Ili kuzitumia fursa hizi kwa tija zaidi, Wizara imeendelea na maandalizi ya Mpango wa Kitaifa wa kutekeleza Diplomasia ya Uchumi. Mpango huo utajumuisha sekta zote husika ikiwa ni pamoja na kuainisha maeneo muhimu ya kisekta yatakayochangia katika kukuza uchumi na Pato la Taifa. Mpango huu utajumuisha pia sekta binafsi na unatarajiwa kukamilika kabla ya mwezi Desemba, 2023.