Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 7 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 121 2023-02-08

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: -

Je, Serikali inawasaidiaje wajane ili kuondoa mila na desturi potofu zinazomkandamiza Mwanamke kwenye suala la mirathi?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Suma Ikenda Fyandomo Mbunge wa viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua uwepo wa wajane na katika kulinda haki zao kwa kutunga Sheria mbalimbali na Kanuni za kulinda haki za Wanawake wajane katika uuala zima la mirathi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mila na desturi potofu ni eneo ambalo Serikali imeanzisha mchakato wa mapitio ya sheria za kimila ili kuondoa aina yoyote ya ukandamizaji kwa wajane katika suala la mirathi. Serikali inaendelea kutoa elimu kuhusu Sheria ya Mirathi hususani umuhimu wa kuandika wosia ili kuondoa changamoto zinazotokana na mila na desturi potofu.