Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 7 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 119 2023-02-08

Name

Mohammed Said Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Konde

Primary Question

MHE.OMAR ALI OMAR K.n.y. MHE. MOHAMMED SAID ISSA aliuliza: -

Je, ni vigezo gani Serikali inavitumia kusamehe kodi ya VAT kwa viwanda mbalimbali nchini ili kuleta usawa kwa wote?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mohammed Said Issa, Mbunge wa Konde kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu wa Msamaha wa Kodi ya Ongezeko la Thamani umewekwa kwa mujibu wa Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani, SURA 148. Sheria imeelezea kwa kina vigezo vinavyotumika kutoa misamaha ya Kodi ya VAT. Vigezo vinavyotumika kusamehe VAT kwa sekta ya viwanda ni kama ifuatavyo: -

i. Uagizaji wa malighafi zinazotumika kutengenezea vyandarua;

ii. Uagizaji au usambazaji wa bidhaa au huduma kwa Serikali zitakazotumika kwenye miradi inayotekelezwa kwa fedha za Serikali, mikopo na misaada kutoka kwa Washirika wa Maendeleo;

iii. Uagizaji au usambazaji wa bidhaa au huduma kwa ajili ya unafuu wa majanga ya asili; na

iv. Uagizaji au usambazaji wa bidhaa au huduma kwa kampuni yenye makubaliano na Serikali katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati, ahsante.