Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 7 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 116 2023-02-08

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji Mwakijembe pamoja na bwawa la kukinga maji?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dunstan Luka Kitandula Mbunge wa Mkinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, skimu ya umwagiliaji inakadiriwa kuwa na jumla ya hekta 450. Hekta 200 katika Kijiji cha Mwakijembe na hekta 250 katika Kijiji cha Mbuta ambazo zinafaa kwa kilimo cha umwagiliaji wa mazao makuu yakiwa ni mahindi, maharage na mbogamboga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imeanza kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina katika skimu zilizopo katika Bonde la Mto Umba ikiwemo skimu ya Mwakijembe kwa lengo la kupata gharama halisi za ujenzi. Baada ya kukamilisha zoezi la upembuzi yakinifu na usanifu wa kina skimu hii itaingia katika mpango wa ujenzi wa mwaka wa fedha 2024/2025.