Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 118 2023-02-08

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: -

Je, ni lini Kijiji cha Kanonge Kata ya Nsimbo kitapelekewa umeme wa REA?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Anna Richard Lupembe, Mbunge wa Nsimbo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kijiji cha Kanoge kilichopo Kata ya Nsimbo kina jumla ya vitongoji vitano vya Kanoge A, Kanoge B, Tupindo, Kavikonge na Tulieni. Kijiji cha Kanoge tayari kimefikiwa na huduma ya umeme katika vitongoji vya Kanoge B na Tulieni. Vitongoji vitatu vilivyosalia vitafikishiwa umeme kupitia Mradi wa kusambaza umeme wa Kitongoji kwa Kitongoji (Hamlet Electrifiction Project) unaotajariwa kutekelezwa nchi nzima kulingana na upatikanaji wa fedha, ahsante.