Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 4 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 66 2023-02-03

Name

Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: -

Je, ni Wananchi wangapi Kondoa Mjini walioharibiwa mazao yao na tembo wamehakikiwa na lini watalipwa?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Juma Makoa, Mbunge wa Jimbo la Kondoa Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kati ya tarehe 25 na tarehe 28 Septemba, 2022, Wizara ilifanya uhakiki wa madai ya kifuta jasho ya wananchi 274 wa Halmashauri ya Mji wa Kondoa walioharibiwa mazao yao na tembo. Baada ya uhakiki huo kukamilika, Wizara iliwalipa wananchi 198 wa Vijiji vya Chemchem, Tungufu, Tampori, Mulua na Iyoli mwezi Novemba, 2022. Jumla ya shilingi 40,013,750 ikiwa ni kifuta jasho kutokana na madhara yaliyosababishwa na wanyamapori.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara imepokea madai mengine mapya ya wananchi 28 wa vijiji vya Unkuku, Kwapakacha, Serya, Damai, Chemchem na Mulua ambayo yamewasilishwa hivi karibuni. Madai hayo yanaendelea kufanyiwa kazi na malipo yatafanyika baada ya taratibu stahiki kukamilika.