Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 4 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 58 2023-02-03

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza: -

Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha mbegu za asili zenye virutubisho zinatambulika kisheria, zinalindwa, zinahifadhiwa na kusajiliwa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Neema Kichiki Lugangira, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeanzisha Kitengo cha Taifa cha Hifadhi ya Nasaba za Mimea chini ya Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) kwa ajili ya kuzitambua na kuzihifadhi nasaba za mimea ikiwemo mbegu za asili za mazao ya kilimo zilizopo nchini. Hadi kufikia Desemba, 2022, sampuli 10,000 ya nasaba za mimea zimekusanywa kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini na kuhifadhiwa katika Benki ya Taifa ya Kuhifadhi Nasaba za Mimea iliyopo Makao Makuu ya TPHPA - Arusha. Serikali imeanza kutekeleza taratibu za kuandaa mapendekezo ya kutunga Sheria ya Hifadhi ya Nasaba za Mimea ambayo itabainisha taratibu za kisheria za kuzitambua, kuzisajili, kuzihifadhi na kutumia mbegu za asili za mazao zilizopo nchini.