Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 2 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 35 2023-02-01

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaboresha kadi ya kliniki ya Watoto chini ya miaka mitano ili kusaidia ufuatiliaji wa wingi wa damu?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Mwanaisha Ng’azi Ulenge, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kadi za kiliniki ya watoto ziliboreshwa tangu mwaka 2011 kwa kuzingatia miongozo ya Shirika la Afya Duniani, ambapo maboresho hayo yamezingatia maeneo yasioacha maeneo hatarishi yoyote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwongozo unaelekeza kutumia mbinu za kitabibu kutambua wingi wa damu kwa mtoto bila kumtoboa na wale wenye dalili za upungufu hupelekwa kwenye vipimo zaidi, ahsante.