Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 2 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 33 2023-02-01

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE K.n.y. MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: -

Je, ni lini mgogoro wa mipaka kati ya Vijiji vya Utengule, Ovindembo, Ipinde, Tanganyika na Kampuni ya Kilombero North's utatatuliwa?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Godwin Emmanuel Kunambi Mbunge wa Jimbo la Mlimba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kampuni ya Uwindaji ya Kilombero North’s Limited imekodishwa Kitalu cha Uwindaji cha Mlimba North’s ambacho ni sehemu ya Bonde la Mto Kilombero. Maeneo ya kitalu hicho ni chanzo muhimu cha maji yanayoingia katika Mto Kilombero ambayo pia yanachangia katika Mradi wa Kitaifa wa kuzalisha umeme wa Bwawa la Mwalimu Nyerere.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Eneo la Kitalu cha Uwindaji cha Mlimba ni moja kati ya maeneo yanayoshughulikiwa na Kamati ya Mawaziri nane inayofanyia kazi migogoro hiyo iliyopo katika vijiji 975. Kufuatia Kamati hiyo, timu ya wataalamu ya Kitaifa inayohusika na utatuzi wa migogoro kwa kushirikiana na Mkoa wa Morogoro na Wilaya za Kilombero, Malinyi na Ulanga imeshakwenda kwenye eneo lenye mgogoro huo kwa lengo la kufanya tathmini na kubaini maeneo halisi yanayostahili kuhifadhiwa kwa maslahi mapana ya Taifa na maeneo mengine wataachiwa wananchi ili waendelee kufanya shughuli zao ikiwemo kilimo, makazi na ufugaji.