Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 22 2023-02-01

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara ya kuunganisha Ruaha Mbuyuni, Malolo hadi Uleling’ombe?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dennis Lazaro Londo, Mbunge wa Mikumi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali barabara hii ya Ruaha Mbuyuni - Malolo hadi Uleling’ombe ilikuwa haijaingizwa katika mtandao wa barabara zinazohudumiwa na TARURA. Serikali kupitia TARURA itatenga fedha kiasi cha shilingi milioni 100 katika mpango na bajeti wa mwaka wa fedha 2023/2024 kwa ajili ya usanifu wa awali wa barabara ya Ruaha Mbuyuni, Malolo mpaka Uleling’ombe yenye urefu wa kilometa 27.9. Lengo la usanifu huo ni kupata gharama halisi za ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha changarawe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mara baada ya kupata gharama halisi za usanifu, Serikali kupitia TARURA itaweka katika mipango yake ya bajeti kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Ruaha Mbuyuni, Malolo hadi Uleling’ombe kulingana na upatikanaji wa fedha.