Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 1 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 12 2023-01-31

Name

Amour Khamis Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbe

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: -

Je, ni kwa nini mizigo ya wasafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar kwa kutumia meli kubwa inapekuliwa na mbwa badala ya scanner?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Amour Khamis Mbarouk, Mbunge wa Tumbe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mizigo yote ya wasafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar kupitia Bandari ya Dar es Salaam inakaguliwa kwa mdaki (scanner). Katika kuimarisha usalama wa bandari, wasafiri pamoja na mizigo inayosafishwa kwenda Zanzibar, Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) iko kwenye hatua za manunuzi ya mdaki (scanner) mwingine mpya kwa ajili ya eneo la meli zifanyazo safari kati ya Dar es Salaam na Zanzibar ili kupunguza muda unaotumika kukagua mizigo na hivyo kufanya eneo hilo kuwa na Midaki miwili. Mdaki mpya unaonunuliwa unatarajiwa kuwasili nchini mwishoni mwa mwezi Aprili, 2023.

Mheshimiwa Spika, matumizi ya mbwa katika Bandari ya Dar es Salaam hufanyika kwa ukaguzi maalum wa mizigo baada ya mizigo hiyo kukaguliwa kwa kutumia mdaki na kuonekana si salama kuruhusiwa kupita, ahsante.