Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 5 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 45 2022-04-12

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza: -

Je, Serikali inachukua hatua gani kudhibiti kuongezeka kwa bei ya mbolea nchini hasa Mkoani Ruvuma?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, bei za mbolea duniani imekuwa ikiongezeka kutokana na kuongezeka kwa gharama za uzalishaji na mahitaji hususan kwenye nchi zenye watumiaji wakubwa wa mbolea kama vile China na India. Ongezeko hilo kwa msimu wa 2021/2022 limechangiwa na athari za UVIKO- 19 na vita kati ya Nchi ya Urusi na Ukraine ambao ni wazalishaji wa malighafi zinazotumika katika utengenezaji wa mbolea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeweka utaratibu wa kudhibiti upandishaji holela wa bei za mbolea kwa kuhusisha Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea nchini, inafanya tathmini ya gharama halisi ya mbolea na kutoa bei elekezi. Mwezi Machi, 2022 Serikali kupitia TFRA imetoa bei elekezi za mbolea za DAP, UREA, CAN na SA katika Mikoa mbalimbali nchini ikiwemo Mkoa wa Ruvuma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuondokana na utegemezi wa uagizaji wa mbolea nje ya nchi, Serikali inaendelela kuvutia uwekazaji wa viwanda vya mbolea hapa nchini. Baadhi ya wawekezaji waliojitokeza ni pamoja na kampuni Itracom inayojenga kiwanda cha mbolea Jijini Dodoma chenye uwezo wa kuzalisha tani 600,000 na Kiwanda cha Minjingu kuendelea na kuongeza uzalishaji kutoka uwezo wa tani 100,000 za sasa hadi kufikia tani 500,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia Bunge lako Tukufu Serikali inasisitiza viongozi wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha kuwa bei elekezi zinazotolewa zinazingatiwa katika vituo vyote vya mauzo ya mbolea. (Makofi)