Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 6 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 56 2022-04-13

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaunda tena Bodi ya Wataalam wa Ugavi na Ununuzi (PSPTB) baada ya kuvunjwa kwa muda mrefu?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Ahmad Pathan, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kufuatia uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi uliofanywa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wizara iliteua Wajumbe wa Bodi ambapo uteuzi wao ulianza Desemba 19, 2021. Ahsante.