Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 6 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 53 2022-04-13

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. HAMIS M. MWINJUMA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa maksudi wa kuwavutia Wawekezaji katika Kilimo cha zao la Muhogo Wilayani Muheza?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hamis Mohamed Mwinjuma, Mbunge wa Muheza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mkakati wa kuendeleza tasnia ya muhogo wa miaka kumi kati yam waka 2020 mpaka mwaka 2030 unaolenga kuimarisha utafiti na uzalishaji wa mbegu bora za zao la muhogo, kuongeza uzalishaji wa muhogo kutoka wastani wa tani 8.2 hadi tani 24 kwa mwaka.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza, Serikali inaendelea na jitihada za kuwavutia wawekezaji ambapo mwaka 2018 kampuni ya CMTL-Tanzania Limited ilipatikana na kupewa eneo la ekari 10 katika Kata ya Mbaramo kwa ajili ya kujenga kiwanda cha kuchakata muhogo. Serikali inafuatilia ili mwekezaji awekeze kulingana na malengo yaliyokusudiwa.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Shirika la MEDA inasambaza jumla ya pingili 700,000 za mbegu za mihogo aina ya Mkuranga 1 na Kiroba katika Halmashauri ya Wilaya ya Muheza kwa ajili ya kupandwa katika eneo la ekari 175.