Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 24 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 202 2016-05-20

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza:-
Serikali ilipandisha hadhi Kituo cha Afya cha Makambako kuwa Hospitali lakini tatizo kubwa lililopo ni ukosefu wa vifaa tiba na kufanya watu wengi kwenda kutibiwa Kibena, Njombe au Ilembula.
Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa hivyo ili watu wasipate taabu ya kwenda kutibiwa Kibena, Njombe au Ilembula?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Kasenyenda Sanga, Mbunge wa Makambako, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kupandisha hadhi Kituo cha Afya Makambako kuwa Hospitali, Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ilitoa vifaa mbalimbali vikiwemo vifaa vya umeme chumba cha upasuaji, kitanda cha kufanyia upasuaji na seti tatu za vifaa vya upasuaji akina mama wajawazito na seti mbili za upasuaji mkubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na jitihada hizo, tukiri kwamba bado upo upungufu wa vifaa kama vile X-ray, Ultrasound, ECG machine na mashine ya dawa za usingizi, pulse oxymeters, monitors, seti ya mashine ya kufulia nguo na vifaa vya meno.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri kwenye bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017 imetenga shilingi milioni 20.9 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba kupitia vyanzo vya mapato ya ndani. Aidha, Halmashauri imepanga kukopa shilingi milioni 154.2 kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba.