Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 9 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 136 2022-11-10

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: -
Je, nini kinakwamisha ujenzi wa barabara ya Mnivata – Masasi kupitia Tandahimba na Newala?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Issa Ally Mchungahela, Mbunge wa Lulindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imepata mkopo wa masharti nafuu kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara kutoka Mnivata hadi Masasi yenye urefu wa kilometa 160. Zabuni kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii zilitangazwa mwezi Julai, 2022 na kufunguliwa tarehe 18 Oktoba, 2022 na kwa sasa uchambuzi wa zabuni unaendelea. Aidha, Serikali imetoa jumla ya Shilingi bilioni 3.086 kwa ajili ya kulipa fidia wananchi watakao athirika na ujenzi huo, na zoezi la kulipa wananchi hao fidia linaendelea. Ahsante.