Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 9 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 130 2022-11-10

Name

Mohammed Said Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA K.n.y. MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha TBS na ZBS zinafanya kazi kwa ushirikiano?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Said Issa, Mbunge wa Jimbo la Konde, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na Taasisi ya Viwango Zanzibar (ZBS) wana hati ya makubaliano (Memorandum of Understanding) iliyosainiwa Mei, 2015 kwa kipindi cha miaka mitano na pia imehuishwa tena mwaka 2020.

Mheshimiwa Spika, katika makubaliano haya yanajikita katika maeneo yafuatayo: -

(i) Uandaaji wa viwango vya Kitaifa;
(ii) Udhibiti wa ubora na usalama wa bidhaa;
(iii) Huduma za metrolojia na upimaji;
(iv) Mafunzo ya kitaalam kwa maafisa wa ZBS; na
(v) Kutambua bidhaa zilizothibitishwa ubora baina ya mashirika haya mawili.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.