Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 8 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 125 2022-11-09

Name

Juliana Didas Masaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA K.n.y. MHE. JULIANA D. MASABURI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapa Vichanja vya kuanikia dagaa Wanawake Wajasiriamali wa Mkoa wa Mara?

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juliana Didas Masaburi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imedhamiria kukuza na kuendeleza zao la dagaa na kuliongeza thamani ili liwe moja ya zao kuu la kimkakati litakalochangia katika kuongeza fursa za ajira, usalama wa chakula na lishe na kukuza uchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kutimiza azma hiyo, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Wizara inatekeleza programu maalum kwa kutumia fedha za mkopo uliotolewa kupitia dirisha la Extended Credit Facility kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa; ambapo shilingi bilioni 1.25 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya ubaridi na mitambo ya kuzalisha barafu kwenye masoko saba ya mazao ya uvuvi na ujenzi wa vichanja vya kukaushia dagaa katika mialo mitatu ya kupokelea samaki.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaangalia uwezekano wa kuwajengea vichanja vya kuanikia dagaa wanawake wajasiriamali wa Mkoa wa Mara katika awamu ya pili ya utekelezaji wa programu hiyo.