Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 8 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 124 2022-11-09

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani kudhibiti tembo wanaovamia Vijiji vya Doroto, Kitaraka, Kamenyanga, Gurungu, Muhanga na Njirii?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Jimbo la Manyoni Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kunusuru maisha na mali za wananchi katika Vijiji vya Doroto, Kitaraka, Kamenyanga, Gurungu, Muhanga na Njirii-Manyoni. Aidha, Wizara imeanza kuimarisha Kituo cha Askari cha wanyamapori kilichopo Kijiji cha Doroto kwa kuongeza Askari, vitendea kazi na kutoa Elimu kwa wananchi juu ya mbinu rafiki za kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu.