Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 8 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 110 2022-11-09

Name

Rashid Abdalla Rashid

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiwani

Primary Question

MHE. RASHID ABDALLA RASHID aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaviwezesha vikundi vya uhifadhi mazingira Vijiji vya Chwaka, Kiwani, Jundamiti, Mwambe, Nanguji na Kendwa?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira naomba kumjibu Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Kiwani. kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tayari imeshachukua hatua za kuvijengea uwezo vikundi vyote vilivyotajwa ili viweze kukua na kujiendesha vyenyewe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, kuvipatia mafunzo ya awali yanayohusu taratibu za uendeshaji na uendelezaji wa vikundi vya ushirika.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, Serikali kupitia Idara ya Vyama vya Ushirika, Zanzibar imepanga kutoa mafunzo kwa Baraza la Wanaushirika la Wilaya ya Mkoani katika robo ya pili ya mwaka huu wa fedha (Oktoba – Disemba 2022).

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar imekuwa na utaratibu wa kutoa mafunzo mbalimbali ya uhifadhi wa mazingira kwa vikundi vya mazingira pamoja na kuwapatia tunzo ya mazingira na vifaa vya usafi kwa vikundi vinavyofanya vizuri katika uhifadhi wa mazingira, Unguja na Pemba.