Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 7 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 91 2022-11-08

Name

Simai Hassan Sadiki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nungwi

Primary Question

MHE. HASSAN SADIKI SIMAI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza malalamiko ya muda mrefu ya ucheleweshwaji wa fedha za Mfuko wa Maendeleo wa Jimbo upande wa Tanzania Zanzibar?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Hassan Sadiki Simai Mbunge wa Nungwi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imechukua jitihada kuhakikisha kuwa fedha za Mfumo wa Kuchochea Maendeleo ya Jimbo zinawasilishwa kwenye majimbo ya Zanzibar kwa wakati. Mtiririko wa uwasilishwaji wa fedha hizo umekuwa wa kuridhisha. Kwa mwaka 2022/2023 shilingi bilioni 1,400,000,000 zimepelekwa Zanzibar mwezi Septemba, 2022. Aidha, fedha za mwaka 2021/2022 zilipelekwa Zanzibar mwezi Oktoba, 2021. Nakushukuru.