Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 3 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 30 2022-04-08

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatatua migogoro ya mikataba ya minara ya simu kati ya kampuni za simu na Kijiji cha Namuchinka Kata ya Kapele?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Condester Michael Sichalwe, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kijiji cha Namchinka kina minara miwili iliyojengwa na Kampuni ya Tigo na Halotel. Minara hiyo imesimikwa katika ardhi inayomilikiwa na watu binafsi na siyo kijiji. Hivyo, watoa huduma hulipa malipo ya pango la ardhi kwa wamiliki hao kulingana na makubalino katika mikataba waliyoingia.

Mheshimiwa Spika, kupitia Bunge lako Tukufu nitoe maelekezo kwa watoa huduma wote kuhakikisha kuwa wanashirikisha Serikali ya Wilaya na Kijiji wanapotaka kujenga minara ya mawasiliano katika Kijiji husika ili kuepuka migogoro inayoweza kujitokeza ya namna hii. Vilevile, watoa huduma wahakikishe waingie mikataba ya ulinzi wa minara na Serikali za Vijiji ili kuwa na ulinzi wa uhakika katika minara ya mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, nitoe rai kwa wananchi kuwa wazalendo na kutoa ushirikiano kwa watoa huduma wakati wa ujenzi na ulinzi wa miundombinu ya mawasiliano ili kuhakikisha huduma za mawasiliano zinakuwa endelevu kwenye maeneo yetu.