Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 3 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 29 2022-04-08

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Igawa hadi Tunduma kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Suma Ikenda Fyandomo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Igawa hadi Tunduma yenye urefu wa kilometa 218 ikiwa ni maandalizi ya kufanyia ukarabati kwa kiwango cha lami. Kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ilikamilika mwezi Agosti, 2021. Aidha, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina umejumuisha barabara ya mchepuo katika Jiji la Mbeya kipande cha Uyole – Songwe Bypass yenye urefu wa kilometa 48.9.

Mheshimiwa Spika, Serikali itafanya ukarabati na upanuzi wa Barabara ya Igawa hadi Tunduma kwa awamu, ambapo awamu ya kwanza itahusisha upanuzi wa barabara kutoka njia mbili kuwa njia nne kwa sehemu ya Uyole – Ifisi yenye urefu wa kilometa 29 ili kupunguza msongamano katika Jiji la Mbeya. Taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi zinaendelea na inatarajiwa kazi itaanza mapema katika mwaka wa fedha 2022/2023.

Aidha, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ukarabati wa sehemu iliyobaki pamoja na kujenga Barabara ya Mchepuo ya Uyole – Songwe bypass. Ahsante. (Makofi)