Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 3 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 26 2022-04-08

Name

Khadija Shaaban Taya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHADIJA S. TAYA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Sensa ya Watu na Makazi inajumuisha takwimu za watu wenye ulemavu na aina ya ulemavu?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Khadija Shaaban Taya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, dodoso la sensa ya watu na makazi itakayofanyika nchini mwezi Agosti, 2022 limejumuisha maswali 10 yanayohusu hali ya ulemavu. Maswali hayo yataulizwa kwa watu wote ikijumuisha umri, jinsi na ulemavu na hivyo kutoa takwimu za hali ya ulemavu nchini. Kupitia sensa hiyo, ni matarajio yetu kuwa Serikali itapata takwimu rasmi za hali ya ulemavu nchini kwa maeneo ya kiutawala, jinsi, hali ya ndoa, kiwango cha elimu, ajira na viashiria vingine muhimu vilivyoainishwa katika dodoso la sensa.

Mheshimiwa Spika, naomba kutumia fursa hii kutoa wito kwa Waheshimiwa Wabunge wenzangu kuungana na Serikali kuwahimiza wananchi kushiriki kikamlifu katika Sensa ya Watu na Makazi itakayofanyika Agosti, 2022 - Sensa kwa Maendeleo, jiandae kuhesabiwa.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.