Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 1 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 8 2022-04-05

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kuu ya Mwanza - Shinyanga kwa kiwango cha njia nne kutoka Mwanza Mjini hadi Usagara?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Shing’oma Mabula, Mbunge wa Nyamagana, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza maandalizi kwa ajili ya ukarabati wa barabara kuu ya Mwanza, Shinyanga, yenye urefu wa kilometa 104 ambao utahusisha na upanuzi wa barabara kutoka njia mbili kuwa njia nne kwa sehemu ya kutoka Mwanza Mjini hadi Usagara, kilometa 25. Kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ukarabati na upanuzi wa barabara hii iko katika hatua za mwisho na inatarajiwa kukamilika tarehe 27 Aprili, 2022.

Mheshimiwa Spika, baada ya usanifu wa kina kukamilika na gharama za ukarabati kujulikana, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ukarabati utakaohusisha upanuzi wa sehemu ya kutoka Mwanza Mjini hadi Usagara, kilometa 25 kutoka njia mbili kuwa njia nne. Ahsante.