Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 7 2022-04-05

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: -


Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Vituo vya Polisi katika Tarafa za Kipatimu, Njinjo na Nanjilinji Wilayani Kilwa?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Francis Kumba Ndulane, Mbunge wa Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kujenga vituo vya Polisi katika maeneo mbalimbali nchini ili kuhudumia wananchi katika kudhibiti uhalifu. Katika Tarafa ya Nanjilinji kinajengwa kituo cha Polisi kitakachogharimu shilingi 67,700,000. Kituo hiki kiko kwenye hatua ya umaliziaji ambapo jumla ya shilingi 62,000,000 zimetumika. Wizara kupitia Jeshi la Polisi itatenga kiasi cha shilingi 5,700,000 ili kukamilisha ujenzi huo kama njia ya kuunga mkono juhudi za wananchi waliochangia ujenzi huo.

Mheshimiwa Spika, Serikali inashauri wananchi wa Tarafa za Kipatimu na Njinjo kutenga maeneo ya kujenga vituo vya polisi na kuanza ujenzi na Serikali itaunga mkono kama ilivyofanya katika Tarafa ya Nanjilinji.