Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 6 2022-04-05

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kununua magari ya Polisi kwa ajili ya vituo vya Polisi nchini?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zuena Athumani Bushiri, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu na uhitaji wa kulipatia Jeshi la Polisi magari kama nyenzo za kutendea kazi. Kupitia mkataba kati ya Serikali na Kampuni ya Ashok Leyland ya nchini India, Serikali inategemea kupokea magari 369 kutoka nchini India ifikapo Septemba, 2022 ambapo mwishoni mwa mwezi Aprili, 2022 tunatarajia kupokea magari 78 yameshakaguliwa na kuthibitishwa. Magari hayo yatakapofika yatagawiwa kwenye Vituo vya Polisi vyenye uhitaji mkubwa.