Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 10 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 149 2022-11-11

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka vifaa kingaradi katika eneo la Mwese lenye milipuko ya radi mara kwa mara?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Moshi Selemani Kakoso, Mbunge wa Mpanda Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kuwa kuna maeneo yenye matukio mengi na makubwa ya radi hususan eneo la Mwese Mkoani Katavi. Hali hii husababisha nguzo nyingi za umeme, transfoma na vifaa vingine vya umeme kuharibiwa na radi.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022 Serikali imetenga shilingi milioni 502 kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya umeme katika Mkoa wa Katavi ikiwa ni pamoja na ununuzi wa nguzo za zege, transfoma zenye kuhimili madhara ya radi (surge arresters) na kuweka waya (overhead shield wire) katika maeneo yenye matukio ya milipuko ya radi mara kwa mara ikiwemo kingaradi eneo la Mwese, ahsante.