Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 10 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 145 2022-11-11

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: -

Je, lini Serikali italeta muswada wa sheria wa kuweka ukomo wa upelelezi kwenye kesi za mauaji nchini?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria napenda kujibu swali la Mheshimiwa Edwin Enosy Swalle, Mbunge wa Lupembe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kesi za mauaji zinaangukia katika makosa makubwa (capital offences) zikiambatana na adhabu kubwa ambayo ni kunyongwa hadi kufa au kifungo cha maisha pale mtu anapopatikana na hatia. Hivyo upelelezi wake unahitaji muda na umakini mkubwa ndiyo maana kwa sasa upelelezi haujawekewa ukomo wa kisheria.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo Mkurugenzi wa Mashtaka kwa mamlaka aliyopewa chini ya Sheria ya Mashtaka katika kuratibu na kusimamia upelelezi wa makosa ya jinai ametoa Mwongozo wa Mkurugenzi wa Mashtaka Na. 1 wa mwaka 2022 kuhusu ufunguaji wa mashtaka na ukamilishaji wa upelelezi wa kesi za jinai uliotolewa tarehe 30 Septemba, 2022 na kuanza kutumika tarehe 1 Oktoba, 2022. Mwongozo huo unataka upelelezi wa kesi za mauaji ambazo hazihitaji utaalam kutoka taasisi nyingine usichukue zaidi ya siku 60 na zile zinazohitaji utaalamu kutoka taasisi nyingine usichukue zaidi ya siku 90. Ahsante.