Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 10 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 144 2022-11-11

Name

Asya Sharif Omar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya usafiri katika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Asya Sharif Omar, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022 Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba umepatiwa magari matatu yaliyonunuliwa na Serikali ili kupunguza uhaba wa magari katika Mkoa huo. Serikali itaendelea kununua magari na pikipiki kila mwaka na kuzigawa katika Mikoa na Wilaya zenye uhitaji mkubwa ikiwemo Mkoa wa Kaskazini na Kusini Pemba. Nashukuru.