Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 10 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 142 2022-11-11

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza: -

Je, ni nini kinakwamisha barabara ya Magamba – Mtapenda – Kasokola hadi Ifukutwa kuhamishiwa TANROADS?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Magamba – Mtapenda - Kasokola hadi Ifukutwa ni mojawapo ya barabara iliyopendekezwa na Kikao cha Kumi na Nane cha Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Katavi kilichofanyika tarehe 23 Februari, 2022 kupandishwa hadhi kuwa barabara ya Mkoa.

Mheshimiwa Spika, Mwenyekiti wa Kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Katavi kwa maana ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi alimwandikia barua Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi barua yenye Kumb. Na FA.364/423/01“C”/29 ya tarehe 11 Oktoba, 2022 kuomba kibali cha kupandishwa hadhi barabara za Wilaya ikiwemo barabara ya Magamba – Mtapenda - Kasokola hadi Ifukutwa kuwa barabara za Mkoa. Mkoa utajulishwa na Waziri mwenye dhamana na barabara kupitia Gazeti la Serikali endapo imekidhi vigezo.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, Serikali kupitia TARURA tutaendelea kuihudumia barabara hii kwa kutenga fedha kwenye bajeti zetu ili iweze kupitika muda wote kulingana na upatikanaji wa fedha.